Kiungo nyota wa kimataifa wa Uingereza na klabu ya Chelsea, FRANK LAMPARD kuna hatihati ya kutocheza mchezo wa kufuzu michuano ya Kombe la Dunia 2014 dhidi ya San Morino Ijumaa ijayo baada ya kuumia katika mchezo ambao timu yake iliibuka kidedea kwa kuifunga mabao 4-1 Norwich.
COLE KUCHUKULIWA HATUA CHELSEA.


Mabingwa mara sita wa Afrika, Al Ahly ya Misri wamelazimishwa sare ya mabao 3-3 na Sunshine Stars ya Nigeria katika mchezo wa kwanza wa nusu fainali ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya iliyochezwa katika Uwanja wa Dipo Dina mjini Ijebu-Ode, Nigeria. Katika mchezo huo Sunshine ilimkosa nahodha wake GODFREY OBOABONA ambaye alikuwa akitumikia adhabu baada ya kuonyeshwa kadi mbili za njano katika wa mwisho wa hatua ya makundi dhidi ya Esperance wakati MOHAMED ABOUTRIKA naye alikosa mchezo huo baada ya kufungiwa miezi miwili na klabu yake ya Al Ahly. Katika mchezo huo mabao ya Al Ahly yalifungwa na MOHAMED NAGY aliyefunga mabao mawili na MAHDY EL SAYED huku mabao ya Sunshine yalifungwa na TAMEN MEDRANO, DELE OLORUNDARE kwa njia ya penati na PRECIOUS OSASCO. Nusu fainali nyingine inatarajiwa kuchezwa leo jijini Lubumbashi ambapo mabingwa mara mbili TP Mazembe itaikaribisha Esperance ya Misri ambapo washambuliaji nyota wa kimataifa kutoka Tanzania MBWANA SAMATTA na THOMAS ULIMWENGU wanatarajiwa kuingoza Mazembe kuibuka na ushindi katika mchezo huo.
_____________________________________________________________
TAARIFA MBALIMBALI KUTOKA TFF LEO.
MISRI NAYO YAIKACHA SERENGETI BOYS
Timu ya Taifa ya vijana wenye umri chini ya miaka 17 (Serengeti Boys) imefuzu kucheza raundi ya tatu nay a mwisho kwenye michuano ya kutafuta tiketi ya kucheza Fainali za Afrika kwa Vijana baada ya Misri kujitoa. Serengeti Boys ilikuwa icheze raundi ya pili dhidi ya Misri; mchezo wa kwanza ukichezwa Oktoba 14 mwaka huu jijini Dar es Salaam na ule wa marudiano wiki mbili baadaye jijini Cairo. Katika raundi ya kwanza Serengeti Boys inayofundishwa na Jakob Michelsen kutoka Denmark ilikuwa icheze na Kenya mwezi uliopita, lakini nchi hiyo ilijitoa katika michuano hiyo ambayo fainali zake zitachezwa Machi mwakani nchini Morocco. Serengeti Boys sasa itacheza raundi ya tatu kwa kumkabili mshindi wa mechi kati ya Zimbabwe na Congo Brazzaville. Mechi ya kwanza itachezwa Novemba 18 mwaka huu jijini Dar es Salaam wakati ya marudiano itafanyika ugenini wiki mbili baadaye. Zimbabwe na Congo Brazzaville zitapambana zitapambana kati ya Oktoba 12-14 mwaka huu, Zimbabwe ikiwa mwenyeji wa mechi ya kwanza wakati ya marudiano itafanyika kati ya Oktoba 26-28 mwaka huu.
LIGI KUU YAINGIA RAUNDI YA SITA
Michuano ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kuwania ubingwan wa Tanzania Bara inaingia raundi ya sita wikiendi hii kwa mechi saba. Kesho (Oktoba 6 mwaka huu) African Lyon itakuwa mwenyeji wa Azam katika mechi itakayochezwa Uwanja wa Azam Complex, Dar es Salaam kuanzia saa 10 kamili jioni. Nayo Ruvu Shooting itaikaribisha Coastal Union ya Tanga katika mechi itakayochezeshwa na Oden Mbaga wa Dar es Salaam kwenye Uwanja wa Mabatini ulioko Mlandizi mkoani Pwani. Mbaga atasaidiwa na Samuel Mpenzu, Ferdinand Chacha na Andrew Shamba. Jumapili (Oktoba 7 mwaka huu) kutakuwa na mechi kati ya Simba na Oljoro JKT itakayochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Kagera Sugar na Yanga (Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba), Mgambo Shooting na Polisi Morogoro (Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga), Toto Africans na JKT Ruvu (Uwanja wa Kirumba jijini Mwanza) na Tanzania Prisons na Mtibwa Sugar (Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya).
No comments:
Post a Comment