
Ikiwa zimepita siku chache tangu tasnia ya filamu nchini Nigeria kumpoteza mkongwe wake marehemu Peter Eneh,Leo tarehe 5 mwezi wa kumi na mbili mwaka 2012 wapenzi wa filamu nchini Nigeria na duniani kwa ujumla wameingia simanzi baada ya kumpoteza veteran mwingine katika tasnia hiyo.
Marehemu Enebeli Elebuwa pichani alikuwa akiwakilisha vema nchi yake kupitia filamu amekufa mapema leo asubuhi huko Newdelhi India alikokuwa amelazwa kwa ugonjwa wa
kupalalaizi alioupata mapema mwaka jana.
Enebeli alizaliwa miaka 65 iliyopita katika mji wa Otagunu huko Nigeria na alianza rasmi kuigiza mwaka 1967 na baadhi ya filamu alizowahi kucheza ni ''lost kingdom,Abuja connection,sensitional,Men do cry na nyingine nyingi.
''R.I.P ENEBELI ELEBUWA''
No comments:
Post a Comment