Amesema: “Si haki kwani baadhi ya Timu
zishacheza, kwa mfano na Newcastle, na nyingine bado kukutana nayo
halafu wanacheza nao huku wakiwa na Wachezaji 6 au 8 wapya!”
Aliongeza: “Nadhani Uhamisho huu ufutwe au Klabu zisinunue Wachezaji zaidi ya wawili!”
Mtindo wa Madirisha ya Uhamisho ulianzishwa kwenye Msimu wa 2002/03.

Katika Kipindi hiki cha Uhamisho Arsenal
haijasaini Mchezaji yeyote mbali ya kuvumishwa kutaka kuwachukua David
Villa wa Barcelona na Mohamed Diame wa West Ham Wachezaji ambao Wenger
amekanusha kujaribu kuwachukua.

Akitolea mfano wa Newcastle ambao kwenye
Dirisha hili la Uhamisho wa Mwezi Januari tayari limewanasa Massadio
Haidara, Yoan Gouffran, Mapou Yanga-Mbiwa na Mathieu Debuchy huku Moussa
Sissoko kutoka Klabu ya Toulouse akiwa njiani kujiunga, Wenger alisema:
“Timu ambazo hazijacheza na Newcastle hazitakutana na Timu ile ile!”
Hadi sasa Wenger hajafuta kuwa hawezi
kusaini Mchezaji mpya Mwezi huu lakini amekiri kuwa akitokea Mchezaji
mzuri ambaye anapatikana watamchukua tu.
Wenger amesisitiza: “Kitu ambacho
kinanitatiza ni kuwapata tena majeruhi wetu na kuwafanya Wachezaji wote
wacheze kwa uwezo wao wote. Hatutegemei miujiza toka nje, tunategemea
mafanikio toka ndani ya Klabu. Ikitokea Mtu anaweza kuimarisha Kikosi
chetu tutamchukua tu lakini kwa sasa tuna Wachezaji wawili kwa kila
pozisheni na hiyo inatosha! Lakini, tukipata Mchezaji wa kiwango cha juu
Duniani hatukatai kumchukua!”
No comments:
Post a Comment