BUKOBA SPORTS

Monday, January 21, 2013

ROBIN VAN PERSIE ASEMA ILIKUWA SAHIHI KUIKACHA ARSENAL!

Robin van Persie, ametamka kuwa uamuzi wake kuihama Arsenal na kutua Manchester United ulikuwa ni uamuzi sahihi na wa wakati muafaka. Robin van Persie ana hakika kuwa ulikuwa wakati muafaka kwake kuihama Arsenal na kutua Manchester United.

Straika huyo hatari ambaye ameifungia Man United Mabao 22 katika Mechi 28 huku Bao 18 zikiwa kwenye Ligi Kuu England alihamia Old Trafford mwanzoni mwa Msimu huu.
Van Persie, akifurahia mwanzo mzuri na Man United, ametamka: “Arsenal ni Klabu kubwa na Siku zote nilijisikia vizuri kuwa nao lakini baada ya Miaka 8 nilijisikia nitafute changamoto nyingine. Changamoto hii nimeipata Manchester United. Nimezungukwa na Mabingwa.”
Aliongeza: “Nahisi huu ni wakati muafaka kuhamia hapa. Kila Siku inaniambia nilifanya uamuzi sahihi. Sidhani ingekuwa safi kuja mapema. Nimekuja hapa kupata changamoto kubwa. Hakuna kitu kibaya kuhusu Arsenal. Hakuna Mchezaji mkubwa kuliko Klabu, Arsenal Siku zote itakuwepo kugombea Makombe na kuwa juu. Lakini baada ya Miaka 8 nilikuwa tayari kuondoka na kujaribu kitu kipya.”
Akizungumzia kuhusu hali yake tangu atue Old Trafford, Robin van Persie amesema kila Mtu amekuwa mwema kwake na imemsaidia sana kujisikia nyumbani.
Amesema: “Nasikia furaha. Naona vitu ambavyo sijaviona muda mrefu. Nilipotua Arsenal kwa mara ya kwanza niliona vitu toka kwa Dennis Bergkamp na Thierry Henry ambavyo nilikuwa sijaviona maishani. Sasa naviona vitu hivyo tena na hilo linanifanya niwe na furaha.”

No comments:

Post a Comment