BUKOBA SPORTS

Saturday, January 26, 2013

ZAHA AFUZU UPIMAJI AFYA, ASAINI MKATABA NA MANCHESTER UNITED, AJIFUNGA KITANZI MPAKA 2018

KUBAKI CRYSTAL PALACE HADI JULAI!
Wilfried Zaha amefaulu upimaji afya yake Klabuni Manchester United na kusaini Mkataba wa Miaka 5 na Nusu na hivyo kukamilisha Uhamisho wa Pauni Milioni 15 kutoka Crystal Palace.
Zaha, mwenye Miaka 20 ambae ni mzaliwa wa Ivory Coast, Msimu huu atamalizia akiwa Crystal Palace ili kuisaidia Klabu hiyo kufuzu kupanda Daraja na kuingia Ligi Kuu England.
Man United italipa Pauni Milioni 10 mbele na Dau hilo linaweza kupanda na kufikia Pauni Milioni 15 ikitegemea Mechi ambazo Zaha atacheza na mafanikio yake wakati akiwa Old Trafford.
Zaha, ambae alijunga na Crystal Palace akiwa na Miaka 12 tu baada ya Familia yake kuhamia Uingereza yeye akiwa na Miaka minne, anatarajiwa kuitwa kwenye Kikosi cha Englandkitakachocheza na Brazil hapo Februari 6 Uwanjani Wembley.
Msimu uliopita, Zaha ndie alietwaa Tuzo ya kuwa Mchezaji mdogo Bora kwenye Ligi England.


WASIFU WA WILFRIED ZAHA
>KUZALIWA: 10 Novemba 1992 huko Ivory Coast na kuhamia England akiwa na Miaka minne
>POZISHENI: Winga au Straika
>KLABU: Crystal Palace (2009-hadi sasa)
>KUANZA KUCHEZA: Crystal Palace v Cardiff (27 Machi 2010)
>MECHI: 124
>MAGOLI: 15
>TIMU ya TAIFA ENGLAND U-19: Mechi 2
>TIMU ya TAIFA ENGLAND U-19:: Mechi 5
>TIMU ya TAIFA ENGLAND: Mechi 1

No comments:

Post a Comment