BUKOBA SPORTS

Friday, February 22, 2013

EUROPA LEAGUE: NEWCASTLE, TOTTENHAM SPURS, CHELSEA ... ZASONGA MBELE, KIJOGOO LIVERPOOL NJE!!


Jana Huko, Stamford Bridge, Sparta Prague walikuwa wakiongoza kwa Bao 1-0 na kufanya wafungane na Chelsea kwa Bao 1-1, Bao la Eden Hazard la Dakika ya 90 lilifanya Mechi iwe sare 1-1 na Chelsea kusonga kwa jumla ya Bao 2-1 katika Mechi mbili.
Awali, Tottenham na Newcastle, zilizokuwa zikicheza ugenini, zote zilifuzu kuingia Raundi ya Mtoano ya Timu 16.
Tottenham ilitoka sare 1-1 na Lyon na Newcastle kuifunga Metalist Kharkiv 1-0.
Huko ANFIELD mambo yalikuwa magumu sana licha ya Suarez kung’ara kwa kupiga Bao 2 safi na kuipa Liverpool ushindi wa Bao 3-1 dhidi ya Zenit St Petersburg ambao Bao lao lilifungwa na Straika hatari Mbrazil Hulk, na hilo ndio Bao lililowaua Liverpool kwani baada ya Mechi mbili Mabao yalifungana kuwa 3-3 na Bao la ugenini la Hulk kuitupa nje ya EUROPA LEAGUE Liverpool.
Mountain: Hulk's goal meant Liverpool needed four goals to progress to the last 16
Goli la Hulk liliwaua Liverpool mara mbili na kuwapandishia deni la magoli
Comeback: Liverpool still needed two goals after half-time if they were to win the tie
 Liverpool mpaka mapumziko walihitajika kufunga goli mbili ili kujihakikishia
Out: Liverpool couldn't score a fourth goal after Suarez's free-kick and were eliminatedSuarez akishangilia baada ya kufunga goli la pili.
Pia, waliokuwa Mabingwa watetezi wa Kombe hili, Atletico Madrid, walibwagwa nje ya EUROPA LEAGUE licha ya kuifunga ugenini Rubin Kazan Bao 1-0 kwa Bao la Dakika ya 85 la Falcao, kwa vile walifungwa 2-0 katika Mechi ya kwanza.
Kabla ya Mechi hizi za Raundi hii, kila Timu ilikuwa ikijua nani atakuwa mpinzani wake endapo wakitinga Raundi ya Mtoano ya Timu 16.
Take that: Shola Ameobi sticks his tongue out after scoring the decisive goal in the tie
Shola Ameobi akishangilia.Cold? Metalist fans took their shirts off while chanting
FC Metalist Kharkiv's mashabiki walikuwa nongwa kwa timu ya Newcastle, kelele nyingi zikiandamwa na usumbufu wa hapa na pale ... lakini Newcastle waliweka pamba masikioni na kuendelea na mtanage na hatimaye kuibuka na ushindi jana usiku kwenye Europa ligi.


RAUNDI IJAYO: KUCHEZWA MACHI 7 na 14
EUROPA LEAGUE LAST-16 DRAW
Anzhi Makhachkala vs Newcastle
Basle
vs Zenit St Petersburg
Benfica
vs Bordeaux
Levante
vs Rubin Kazan
Steaua Bucharest
vs Chelsea
Stuttgart
vs Lazio
Tottenham
vs Inter Milan
Viktoria Plzen
vs Fenerbahce

No comments:

Post a Comment