BUKOBA SPORTS

Friday, August 30, 2013

FRANCK RIBERY MCHEZAJI BORA ULAYA 2013, AMFUNIKA MESSI NA CRISTIANO RONALDO!!

MONACO, Ufaransa
WINGA wa Bayern Munich Franck Ribéry ameibuka kidedea katika tuzo ya Mchezaji Bora wa Ulaya kwa mwaka 2013 na kuwabwaga Lionel Messi na Cristiano Ronaldo aliokuwa akichuana nao kwenye kinyang’anyiro hicho.

Katika ghafla hiyo ambayo ilifanyika jijini Monaco, Ufaransa upigaji wa kura za mchezaji bora ulifanyika ‘Live’ na Ribery kuwafunika wawili hao ambao wamekuwa wakitawala soka katika miaka ya karibuni.
Ronaldo hakutokea katika hafla hiyo, ambapo Ribery baada ya kutangazwa mshindi aliwashukuru wachezaji wenzake wa Bayern na familia yake kwa sapoti waliyompa.
Katika hatua nyingine mbali na hafla hiyo pia ilishuhudia upangaji wa makundi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa msimu wa 2013-14.

****************

WACHEZAJI WALIOSHIKA NAFASI ZA 4 HADI 10:
4 Robert Lewandowski (POL) – Borussia Dortmund (Pointi 80)
5 Arjen Robben (NED) – FC Bayern München (55)
6 Thomas Müller (GER) – FC Bayern München (51)
7 Gareth Bale (WAL) – Tottenham Hotspur FC (48)
8 Bastian Schweinsteiger (GER) – FC Bayern München (34)
9 Zlatan Ibrahimović (SWE) – Paris Saint-Germain FC (27)
10 Robin van Persie (NED) – Manchester United FC (24)

No comments:

Post a Comment