Andy Murray
Bingwa mtetezi wa mashindano ya tenisi ya US Open Andy Murray amefanikiwa kutinga hatua ya robo fainali ya mashindano baada ya kumlaza Denis Istomin wa Uzbekistan.
Kwa ushindi huo Andy Murray sasa atakabiliana na Stanislas Wawrinka katika hatua hiyo ya robo fainali siku ya Alhamisi ya wiki hii.
Andy Murray mwenye umri wa miaka 26 alipata wakati mgumu na hatimaye kufanikiwa na ushindi wa seti za 6-7 (5-7) 6-1 6-4 6-4.
Mwonekano mzuri wa uwanja wa Arthur Ashe Arena nyuma ni jua likizama Manhattan
Andy Murray alimsifu mpinzani wake Denis Istomin na kusema kuwa alimpa wakati mgumu kutokana na umahiri wake kimchezo. Mchezaji huyo amesema kuwa kwa sasa anaelekeza nguvu katika mchezo wake wa robo fainali ili apate ushindi katika harakati zake za kutetea ubingwa.
Murray akicheza huku mataa yakimlika mwanga kwenye eneo la Arthur Ashe Stadium
Murray akicheza uwanjani
Mpenzi wa Murray akifurahia baada ya jembe lake kushinda na kutinga hatua ya robo ya michuano hiyo ya US OPEN 2013.
Murray nae akicheka kwa furraha hapa
No comments:
Post a Comment