BUKOBA SPORTS

Thursday, September 12, 2013

FIFA LISTI YA UBORA DUNIANI: SPAIN YABAKI JUU, BONGO TZ JUU NAFASI 1!

FIFA leo imetoa Listi ya Ubora Duniani na Mabingwa wa Dunia, Spain, bado wako pale pale wakishika Nambari Wani huku Tanzania ikipanda Nafasi moja na kushika Nafasi ya 127 lakini kwenye 10 Bora kuna mabadiliko makubwa.

Argentina imeibwaga Germany na kuikamata Nafasi ya Pili, Uruguay imepanda Nafasi 5 na sasa ipo ya 7 huku Portugal ikiporomoka kutoka Nafasi 4 na kutua Nafasi ya 11.
Katika 10 Bora zipo Nchi za Marekani ya Kusini 4.
Kwa Nchi za Afrika, Nchi ambayo iko Nafasi ya juu kabisa ni Ivory Coast ambayo iko Nafasi ya 19 ikiwa imeporomoka Nafasi moja na kufuatiwa na Ghana iliyobaki Nafasi ya 24 kama Mwezi uliopita.


Listi ya Ubora inayofuata itatolewa hapo Oktoba 17.
LISTI YA UBORA YA FIFA:[20 BORA]
1.   Spain
2.  Argentina
3.  Germany
4.   Italy
5.   Colombia
6.    Belgium
7.    Uruguay
8.    Brazil
9.    Netherlands
10.  Croatia
11.   Portugal
12.   Greece
13.   USA
14.   Switzerland
15.   Russia
16.   Chile
17.   England
18.   Bosnia-Herzegovina
19.   Côte d'Ivoire
20.   Ecuador

No comments:

Post a Comment