BUKOBA SPORTS

Monday, September 23, 2013

PAOLO DI CANIO HANA KAZI TENA SUNDERLAND, ATIMULIWA BAADA YA KUSHINDA MECHI 3 TU KATI YA 13.


Sunderland wamemtimua Meneja wao Paolo Di Canio baada ya mwanzo mbovu kwenye Ligi Kuu England ambapo Timu hiyo imejikuta ipo mkiani kwenye Msimamo wa Ligi hiyo.
Tangu ateuliwe kuwa Meneja wa Sunderland Mwezi Machi, Di Canio, mwenye Miaka 45, ameshinda Mechi 3 tu kati ya 13 alizosimamia na Msimu huu ameambua Pointi 1 tu katika Mechi za Ligi 5.
Klabu ya Sunderland imetoa tamko kuwa mrithi wa Di Canio atatangazwa hivi karibuni na kwa sasa Timu hiyo itakuwa chini ya Kocha Kevin Ball.
Mechi ya kwanza chini ya Kocha Kevin Ball itakuwa ni Jumanne watakapocheza Nyumbani Stadium of Light na Peterborough United kwenye Raundi ya Tatu ya Capital One Cup.
Baada ya Mechi hiyo, Sunderland watakuwa Wenyeji kwa Liverpool Jumapili ijayo, kisha kucheza na  Manchester United Oktoba 5 na kufuatia Dabi ya eneo la Wear-Tyne dhidi ya Newcastle hapo Oktoba 27.
Mwezi Machi Mwaka huu, Di Canio alitinga Sunderland kuchukua nafasi ya Martin O'Neill, aliefukuzwa na akakaribishwa na madai kuwa yeye anasapoti Mafashisti.Great result: The Italian won the approval of the fans with a brilliant win over arch-rivals Newcastle at St James' Park
Meneja huyo kutoka Italy mwenye vituko amekuwa mwepesi kuwaponda Wachezaji wake waziwazi Magazetini na hili limeleta mkwaruzo ndani ya Timu.
Msimu huu, Di Canio alianza kwa kipigo cha Nyumbani na Fulham, Sare na Southampton na kisha vipigo toka kwa Crystal Palace, Arsenal na hivi Juzi West Brom.Antics: His passionate touchline antics were appreciated by Sunderland fans
Mbali ya kusaini Wachezaji 14 kwa ajili ya Msimu huu mpya, Di Canio pia aliwauza Wachezaji mahiri
Kama Kipa Simon Mignolet kwa Liverpool na Stephane Sessegnon kwa West Brom ambae hivi Juzi katika Mechi yake kwanza tu na West Brom alifunga Bao walipoicharaza Sunderland 3-0.
Sunderland sasa inasaka Meneja mpya wa 6 katika kipindi cha chini ya Miaka mitano.
Paulo Di Canio aliyezoea kuruka juu na kubanjuka leo hii katimuliwa kazi. Kocha wa Sunderland Paulo Di Canio akiwa kakata tamaa hapa baada ya kipingo cha West Brom.Pressure - Di CanioDi Canio akishangaa baada ya kufungwa na Stephane Sessegnon wikiendi hii.

ANGALIA MITANANGE YOTE ALIYOSIMAMIA SUNDERLAND MPAKA ANAFUKUZWA.
2012-13
April 7 - Chelsea 2  Sunderland 1 (L)
Apr 14 -
Newcastle 0 Sunderland 3 (W)
Apr 20 - Sunderland 1 Everton 0 (W)
Apr 29 - Aston Villa 6 Sunderland 1 (L)
May 6 - Sunderland 1 Stoke 1 (D)
May 12 - Sunderland 1 Southampton 1 (D)
May 19 - Tottenham 1
Sunderland 0 (L)
2013-14
August 17 - Sunderland 0 Fulham 1 (L)
Aug 24 - Southampton 1
Sunderland 1 (D)Aug 27 - Sunderland 4 MK Dons 2 [Capital One Cup] (W)
Aug 31 - Crystal Palace 3
Sunderland 1 (L)September 14 - Sunderland 1 Arsenal 3 (L)
Sep 21 - West Brom 3
Sunderland 0 (L) 


KUHUSU DI CANIO
-KUZALIWA: Rome, 9 Julai 1968
-KLABU ALIZOCHEZA: Lazio, Juventus, Napoli, AC Milan, Cisco Roma, Celtic, Sheffield Wednesday, West Ham, Charlton
-FAINI: £10,000 Mwaka 1998 kwa kumsukuma na kumwangusha Refa Paul Alcock baada ya kutolewa katika Mechi dhidi ya Arsenal
-TUZO YAUCHEZAJI WA HAKI: Mwaka 2001 kwa kudaka Mpira badala ya kufunga ili Kipa wa Everton Paul Gerrard apate Huduma ya Kwanza baada kuumia.
-APONDWA: Mwaka 2005 kwa kutoa Saluti ya Kifashisti kwenye Gemu na Lazio.
-ATEULIWA: Bosi wa Swindon Mei 2011 na kuwapandisha LIGI 1 Mwaka mmoja baadae
-AJIUZULU: Kama Bosi wa Swindon Februari 2013
-AMBADILI: Martin O'Neill kama Meneja wa Sunderland Machi2013 na kuinusuru kushushwa Daraja toka Ligi Kuu England.
-ATIMULIWA: Sunderland baada Mechi 5 za Ligi ambazo amefungwa 4 kati ya hizo na Sare moja.

No comments:

Post a Comment