BUKOBA SPORTS

Tuesday, September 10, 2013

WANAMICHEZO MAARUFU DUNIANI NI WANASOKA, NA RONALDO NDIE JUU!!

KWA MUJIBU wa Takwimu zilizochapishwa leo na Gazeti maarufu huko Ufaransa, L'Equipe,Wanamichezo 6 kati ya 10 maarufu Duniani ni Wanasoka na Cristiano Ronaldo ndie Nambari Wani.

L'Equipe limechukua idadi ya Wapenzi ya kila Mwanamichezo maarufu kwenye Kurasa zao za Mtandao wa Facebook na kuangalia Mwanamichezo yupi kapewa ‘Gonga za Sapoti’, yaani ‘LIKEs’ nyingi, na katika 10 Bora Duniani Wanasoka wako 6, Mpira wa Kikapu watatu na Tenisi mmoja huku Mwanasoka Cristiano Ronaldo akiwa Nambari Wani kwa Likes 60,274,869 akifuatiwa na Lionel Messi mwenye 48,000,104.

TAKWIMU:
JINA MCHEZO FACEBOOK LIKES
C. Ronaldo Soka 60,274,869
Lionel Messi Soka 48,000,104
David Beckham Soka 29,150,690
Michael Jordan MPIRA KIKAPU 23,817,809
Kaka Soka 23,477,568
Kobe Bryant MPIRA KIKAPU 16,693,216
LeBron James MPIRA KIKAPU 14,802,829
Andres Iniesta Soka 14,357,223
Neymar Soka 13,388,531
Roger Federer TENISI 13,289,792

Listi hiyo ya 10 Bora imewabwaga Majina makubwa ya Wanamichezo maarufu kama vile Usain Bolt, Michael Phelps, Sebastian Vettel, Sachin Tendulkar, Tiger Woods, Floyd Mayweather na Rafa Nadal.

Mchezaji ambae Juzi alivunja Rekodi ya kuwa mwenye Bei ghali Duniani, Gareth Bale, yupo Nafasi za chini akiwa na ‘Likes’ chini ya Milioni 5 kwenye Ukurasa wake wa Facebook.

No comments:

Post a Comment