BUKOBA SPORTS

Tuesday, October 15, 2013

SIR ALEX FERGUSON AMWAGIWA SIFA JANA JUMATATU, APEWA ‘UHURU WA MANISPAA YA TRAFFORD!’

LEJENDARI Sir Alex Ferguson, Meneja Mstaafu wa Mabingwa wa England Manchester United, Jana alipewa heshima kubwa Jijini Manchester baada ya kutunukiwa ‘Uhuru wa Manispaa ya Trafford’ na hii ni pamoja na kuubadili Jina Mtaa unaoelekea Uwanjani Old Trafford kutoka Water's Reach na sasa kuwa Sir Alex Ferguson Way.

Heshima hii aliyopewa Sir Alex Ferguson ni kwa kutambua mafanikio yake akiwa na Klabu ya Manchester United kati ya Mwaka 1986 hadi 2013 kipindi ambacho alitwaa Mataji 38.
Sir Alex anafuata nyayo za Lejendari mwingine wa Man United, Sir Matt Busby, ambae Mwaka 1993 Mtaa uitwao Warwick Road North ulibadilishwa Jina na kuitwa Sir Matt Busby Way.

Ferguson, mwenye Miaka 71, tayari anazo heshima nyingine ikiwa ni pamoja na Jukwaa moja la Uwanja wa Old Trafford kuitwa Sir Alex Ferguson Stand na pia Sanamun yake ya Shaba kusimikwa nje ya Uwanja huo.
Huko kwao Scotland, Sir Alex Ferguson ameshapewa ‘Uhuru wa Jiji la Glasgow.’
Hivi sasa, Ferguson ni Mkurugenzi kwenye Klabu ya Man United.

Honour: Sir Alex Ferguson receives the Freedom of the Borough of Trafford from Mayor Dylan Butt (left).
Sir Alex Ferguson receives the Freedom of the Borough of Trafford from Mayor Dylan Butt (left) on Monday. Also pictured are Trafford Council leader Matt Colledge (second left), chief executive Theresa Grant (second right) and Ferguson's wife Cathy (right).
Presentation: Ferguson has been recognised for his achievements in winning 38 trophies in 26-and-a-half years with Man United
Ferguson
Ferguson
Unprecedented success: Ferguson won 38 trophies in his 26-and-a-half years at Old Trafford, including 13 Premier League titles
Ferguson alishinda 38 Old Trafford, ikiwa pamoja na la mara ya 13 Premier League
Place in history: Ferguson guided Man United to another Champions League triumph in 2007 - his second win and the club's third
Ferguson pia aliwawezesha  Man United kushinda kombe la Champions League mwaka 2008

Old friend: Ferguson with the FA Cup after United beat Millwall 3-0 at Cardiff in 2004 - he won the trophy five times
Enzi hizo: Ferguson akiwa amebeba kombe la FA baada ya United kuwafunga Millwall 3-0 kwenye Uwanja a Cardiff mwaka 2004 - akiwa ameshinda mara 5

SIR ALEX: MAKOMBE AKIWA MAN UNITED
LIGI KUU: 1993, 1994, 1996, 1997, 1999, 2000, 2001, 2003, 2007, 2008, 2009, 2011, 2013
FA CUP: 1990, 1994, 1996, 1999, 2004
LEAGUE CUP: 1992, 2006, 2009, 2010
UEFA CHAMPIONZ LIGI: 1999, 2008
UEFA KOMBE LA WASHINDI: 1991
FIFA CLUB WORLD CUP: 2008
UEFA SUPER CUP: 1992
INTER-CONTINENTAL CUP: 1999
FA CHARITY/COMMUNITY SHIELD: 1990, 1993, 1994, 1996, 1997, 2003, 2007, 2008, 2010, 2011

No comments:

Post a Comment