Hili ni pigo kwa Liverpool ambao pia kwa sasa wanamkosa Straika wao mahiri Daniel Sturridge ambae pia ni majeruhi na ambae atakuwa nje kwa Miezi miwili baada kuumia enka.
Habari hizi zitawasumbua sana Liverpool maana ndio wanaingia kwenye kipindi cha Mechi nyingi na mfululizo na Jumapili wanaanza Ugenini kucheza na Tottenham kisha kucheza Nyumbani na Cardiff City na kufuatia Mechi za Ugenini dhidi ya Manchester City na Chelsea, zote zikiwa kabla ya mwisho wa Mwezi huu.
Kwa sasa Liverpool wapo Nafasi ya Pili kwenye Msimamo wa Ligi, wakiwa Pointi sawa na Chelsea na kuwazidi Magoli tu, na wako nyuma ya Vinara Arsenal kwa Pointi 5.
No comments:
Post a Comment