BUKOBA SPORTS

Wednesday, February 12, 2014

COPA DEL REY: RONALDO AFUNGA BAO MBILI NA KUIPELEKA REAL FAINALI!! USIKU HUU NI REAL SOCIEDAD v BARCELONA

BAO 2 za Penati za Cristiano Ronaldo Jana Usiku ziliifanya Real Madrid itinge Fainali ya Copa del Rey baada ya kuibwaga Atletico Madrid kwenye Mechi ya Marudiano ya Nusu Fainali iliyochezwa Estadio Vicente Calderon. Pick that one out: Ronaldo and Real Madrid were off to a flyer at the Vicente Calderon
Penati hizo za Ronaldo zilifungwa Dakika ya 7 na 16 na kuwabwaga nje Atletico Madrid ambao ndio walikuwa Mabingwa Wateteza wa Kombe hili.
Sasa Real wametinga Fainali kwa Jumla ya Bao 5-0 baada kushinda Mechi ya Kwanza 3-0 huko Santiago Bernabeu Wiki iliyopita.
Cutting in: Real playmaker Isco nips across to try and prevent Raul Garcia getting his shot away
Kwenye Fainali Real itacheza na Mshindi wa Leo kati ya Real Sociedad na Barcelona ambao wanarudiana huko Estadio Anoeta huku Barcelona wako mbele kwa Bao 2-0 walizopata huko Nou Camp Wiki iliyopita.
Bale akiendesha!!

Bale akiongea na Ronaldo wakati wa mtange wao na Atletico

Ronaldo akichuana na Miranda pamoja na Emiliano Insua

Ronaldo akishangilia baada ya kufunga bao la pili na mchezo kumalizika 2-0

No comments:

Post a Comment