Tangu Levy aitwae Spurs Mwaka 2001, Mameneja 9 wameshaondoka hapo na wa mwisho ni Tim Sherwood ambae alifukuzwa Juzi Jumanne baada ya kuwa kitini kwa Miezi mitano tu.
Allen, Miaka 52, amemwelezea Levy kama Mafanyabiashara mzuri lakini maamuzi yake ya Kisoka ni mabovu.
Allen amedai: "Sidhani kama yeye ni Mtu wa Soka. Haya maamuzi yatakuja kumsulubu!”
Allen, ambae alikuwa Meneja wa Suprs kwa Mechi 1 tu baada ya kutimuliwa kwa Martin Jol Mwaka 2007, pia ameponda ununuzi wa Wachezaji wa Spurs wa hivi karibuni.
Amesema: “Ni Kikosi chenye thamani kubwa mno na Mtu lazima awajibike. Inasikitisha sana Kikosi hiki kimemaliza Ligi Nafasi ya 6 na hakiwezi kushindana na Timu zilizo 4 Bora. Lazima ufanywe uamuzi wa dira mpya ni ipi!”
Meneja wa mwisho kutimuliwa, Tim Sherwood, alijifananisha na ‘Mwalimu wa Ugavi’ baada Wachezaji wake kuambiwa na Mawakala wao kwamba Meneja huyo hatakuwepo Klabuni hapo Msimu ujao wakati yeye mwenyewe alikuwa hajui lolote kuhusu hatima yake.
Hivi sasa kuna minong’ono kuwa Spurs inalenga kuwaajiri ama Meneja wa Southampton Mauricio Pochettino au Bosi wa Ajax Frank de Boer kuziba pengo la Sherwood.
MAMENEJA CHINI YA LEVY:
-George Graham
-Glenn Hoddle
-David Pleat
-Jacques Santini
-Martin Jol
-Juande Ramos
-Harry Redknapp
-Andre Villas-Boas
-Tim Sherwood
No comments:
Post a Comment