BUKOBA SPORTS

Wednesday, October 22, 2014

UEFA CHAMPIONS LEAGUE: LEO JUMATANO ANFIELD NI MAJOGOO LIVERPOOL vs REAL MADRID

Liverpool v Real Madrid UEFA Champions League Group B 2014/2015 Official Match Programme

UEFA CHAMPIOS LEAGUE baada ya kurudi dimbani jana Jumanne na leo Jumatano kwa Mechi za 3 za Makundi huku Mabingwa wa Ulaya Real Madrid wakitua Anfield kupambana na Liverpool katika Mechi ya Kundi B.Kwenye Kundi hilo, Real wapo kileleni baada ya kushinda Mechi zao zote 2 na wanafuata FC Basel wenye Pointi 3 pamoja na Liverpool na mkiani ni Ludogorets Razgrad ambao hawana Pointi.
Jumanne, Mabingwa wa England, Manchester City, watafungua dimba kwa Mechi ya kwanza kabisa itakayochezwa mapema huko Moscow, Urusi watakapoivaa CSKA Moscow kwenye Mechi ya Kundi E.

Baadae Usiku huo, Chelsea watakuwa kwao Stamford Bridge kucheza na NK Maribor.
Arsenal wao watacheza Jumatano Ugenini huko Uholanzi kwa kuivaa RSC Anderlecht.


Bale wenda mechi hii akawa nje ya Dimba

UEFA CHAMPIONS LEAGUE
RATIBA
Jumatano Oktoba 22

KUNDI A
Atlético Madrid v Malmö FF
Olympiakos v Juventus
KUNDI B
Liverpool v Real Madrid
Ludogorets Razgrad v FC Basel
KUNDI C
Bayer 04 Levserkusen v Zenit St Petersburg
Monaco v Benfica
KUNDI D
Galatasaray v Borussia Dortmund
RSC Anderlecht v Arsenal

No comments:

Post a Comment