BUKOBA SPORTS

Tuesday, November 11, 2014

BAADA YA KICHAPO, ARSENE WENGER: HAKUNA ATAKAEWASHIKA VINARA CHELSEA!

MENEJA wa Arsenal Arsene ameungama kuwa Msimu huu hakuna Timu yeyote itakayowashika Vinara wa Ligi Kuu England amabao baada ya Mechi 11 wanaongoza wakiwa kwa mbele kwa tofauti ya pengo la Pointi 4 mbele ya Timu ya Pili Southampton.
Nyuma ya Southampton wapo Mabingwa Watetezi Manchester City ambao wako Pointi 8 nyuma ya Chelsea.

Jumapili, Arsenal walitwangwa 2-1 na Swansea na sasa wapo Nafasi ya 6 wakiwa Pointi 12 nyuma ya Chelsea.
Wenger ameeleza: “Wakiendelea hivi, inaonyesha hakuna atakaeikamata Chelsea! Kwa sasa hakuna anaeonyesha hivyo!”
Jumamosi, wakiwa huko Anfield, Chelsea walitoka nyuma kwa Bao 1-0 na kuichapa Liverpool Bao 2-1.
Arsenal walipofungwa jumapili na Swansea

Ligi Kuu England sasa imesimama kupisha Mechi za Kimataifa na itarejea tena kilingeni Jumamosi Novemba 22 na Siku hiyo Arsenal wako kwao Emirates kucheza na Manchester United.

No comments:

Post a Comment