Nyuma ya Southampton wapo Mabingwa Watetezi Manchester City ambao wako Pointi 8 nyuma ya Chelsea.
Jumapili, Arsenal walitwangwa 2-1 na Swansea na sasa wapo Nafasi ya 6 wakiwa Pointi 12 nyuma ya Chelsea.
Wenger ameeleza: “Wakiendelea hivi, inaonyesha hakuna atakaeikamata Chelsea! Kwa sasa hakuna anaeonyesha hivyo!”
Jumamosi, wakiwa huko Anfield, Chelsea walitoka nyuma kwa Bao 1-0 na kuichapa Liverpool Bao 2-1.
Arsenal walipofungwa jumapili na Swansea 
Ligi Kuu England sasa imesimama kupisha Mechi za Kimataifa na itarejea tena kilingeni Jumamosi Novemba 22 na Siku hiyo Arsenal wako kwao Emirates kucheza na Manchester United.
No comments:
Post a Comment