BUKOBA SPORTS

Tuesday, November 18, 2014

ED WOODWARD: MANCHESTER UNITED ITASAJILI WALENGWA TUU MWEZI JANUARI!!

MTENDAJI MKUU wa Manchester United Ed Woodward amesema hawatasaini ‘Kiraka’ yeyote Mwezi Januari Dirisha la Uhamisho likifunguka labda ukiwepo uwezekano wa kumsaini Mchezaji mlengwa wao.
Baada ya kutumia zaidi ya Pauni Milioni 150 na pia kuvunja Rekodi ya Klabu kwa kumsaini Angel Di Maria kwa Pauni Milioni 59.7 kutoka Real Madrid mwanzoni mwa Msimu, Ed Woodward amesema hawana papara kusajili Wachezaji wapya.
Amesema: “Hatupo Sokoni kutafuta Kiraka wa muda mfupi. Lakini tunao walengwa wetu tunawaowataka mwishoni mwa Msimu. Ikitokea yeyote kati ya hao anaweza kupatikana Januari, kitu ambacho adimu, tutachukua hatua. Lakini uwezekano ni finyu.”
Mwanzoni mwa Msimu, Man United iliwanunua Ander Herrera (£28m), Luke Shaw (£27m), Marcos Rojo (£16m), Daley Blind (£13.8m) na Pia kutumia £6m kumchukua Radamel Falcao kwa Mkopo.

No comments:

Post a Comment