BUKOBA SPORTS

Sunday, January 25, 2015

UHAMISHO: KLABU YA VILLAREAL YAMUUZA GABRIEL PAULISTA KWA ARSENAL KWA DAU LA £15million, JOEL CAMPBELL ABEBWA KWA MKOPO!

Klabu ya Spain Villarreal imetangaza kuwa imefikia makubaliano ya awali na Arsenal ili kuwauzia Sentahafu wao Gabriel Paulista huku Fowadi wa Arsenal, Joel Campbell, akienda kwa Mkopo Villareal hadi mwishoni mwa Msimu.

Awali Villareal walitaka Arsenal iwalipe Pauni Milioni 15 ili kukidhi Kipengele cha Mkataba wa Paulista cha kumruhusu kuondoka kabla Mkataba wake kumalizika lakini Arsenal walikuwa tayari kutoa Pauni Milioni 10 tu.
Hata hivyo, Uhamisho huu wa Paulista huenda ukanasa kupata Kibali cha Kazi Nchini Uingereza kutokana na Beki huyo mwenye Miaka 24 kutowahi kuichezea Timu ya Taifa ya Brazil.

No comments:

Post a Comment