BUKOBA SPORTS

Sunday, February 8, 2015

VODACOM PREMIER LEAGUE: YANGA 2 vs 0 MTIBWA SUGAR, MRISHO NGASSA AIPANDISHA YANGA KILELENI!!


Mshambuliaji wa Yanga, Haruna Niyonzima (kushoto) akichuana na beki wa Mtibwa Sugar, David Luhende wakati wa mchezo wa Ligi Kuu ya soka Tanzania Bara uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Yanga ilishinda 2-0.
Yanga wameinyuka Mtibwa Sugar bao 2-0 leo kwenye Uwanja wa Taifa Jijini Dar es salaam na kupanda kileleni mwa Ligi kwa pointi 25 na wakiwa na mchezo mmoja mkononi. Mwamuzi ni wa mchezo huu alikuwa ni Israel Mujuni, Mfungaji wa bao zote mbili ni Mrisho Alfan Ngassa.

Beki wa Mtibwa Sugar, Shaban Nditi akimdhibiti beki wa Yanga, Mbuyu Twite.

Kocha wa Yanga, Hans Pluijm akitoa maelekezo kwa wacherzaji wakei.

Mshambuliaji wa Yanga, Amis Tambwe akichuana na kipa wa Mtibwa Sugar, Said Mohamed wakati wa mchezo wa Ligi Kuu ya soka Tanzania Bara uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Yanga ilishinda 2-0. (Picha na Francis Dande)

Mshambuliaji wa Yanga, Amis Tambwe akichuana na kipa wa Mtibwa Sugar, Said Mohamed wakati wa mchezo wa Ligi Kuu ya soka Tanzania Bara uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Yanga ilishinda 2-0.

Mshambuliaji wa Yanga, Simon Msuva akimpiga chenga kipa wa Mtibwa Sugar, Said Mohamed hata hivyo Msuva baada ya kubaki na goli alipiga nje mpira huo.

Msuva akikosa bao.

Msuva akijilaumu baada ya kukosa bao la wazi.

Kikosi cha Mtibwa Sugar.

Kikosi cha Yanga.

Benchi la ufundi la Mtibwa Sugar.

Kipa wa Mtibwa Sugar, Said Mohamed akiwapanga wachezaji wake.
Mashabiki wa Yanga wakifuatilia mchezo huo.

No comments:

Post a Comment