Wiki 3 baadae, Atletico ikaifunga tena Real 1-0 ndani ya Nyumba ya Real, Santiago Bernabeu, katika Mechi ya La Liga na kisha kuitoa Jumla ya Bao 4-2 katika Mechi mbili za Copa del Rey Mwezi Januari ambazo Atleti ilishinda 2-0 kwao na Sare 2-2.
Baada ya hiyo kikaja kichapo cha 4-0 alichopewa Real kwenye La Liga Mwezi Februari na Wiki iliyopita ndio ikaja Sare ya 0-0 huko Vicente Calderon katika Mechi ya Kwanza ya Robo Fainali ya UEFA CHAMPIONS LIGI.
Lakini Real wanatinga kwenye Mechi hii wakiwa na upungufu wa Wachezaji wao muhimu kina Marcelo, ambae yuko Kifungoni, na Kiungo Luka Modric na Fowadi Gareth Bale ambao ni Majeruhi, huku kukiwa na hatihati kama Karim Benzema atacheza kwani ana maumivu ya Enka.
Nao Atletico huenda wakamkosa Fowadi wao hatari Mario Mandzukic ambae anauguza Enka na akikosekana basi Mtoto wa Nyumbani Fernando Torres atavaa Jezi.
Robo Fainali-Mechi za Marudiano
Mechi zote mbili kuanza Saa 3 Dakika 45 Usiku
Jumatano Aprili 22
Real Madrid vs Atletico Madrid [Santiago Bernabeu, Madrid, Spain] [0-0]
AS Monaco vs Juventus [Stade Louis II, Monaco, France] [0-1]
No comments:
Post a Comment