Mserbia mwenye umri wa miaka 28 alithibitisha udedea wake alipomlamza Murray seti tatu kwa nunge za alama 6-1 7-5 7-6 (7-3).
4 kati ya hizo mikononi mwa mtani wake wa jadi Djokovic .
Kwa upande wake Djokovic alisajili ushindi wake wa 6 mjini Melbourne na sasa anatoshana nguvu na bingwa wa zamani Roy Emerson kutoka Australia.
Murray, 28, sasa ameingia katika kumbukumbu kwa kushindwa katika fainali 5 za Grand Slam za tenis tangu kuasisiwa kwa mashindano hayo ya wazi mwaka wa 1968.
Murray alifululiza moja kwa moja hadi kwenye uwanja wa ndege ambapo anatarajiwa kujiunga na mkewe anapojifungua wakati wowote kutokea sasa.
Endapo Mserbia huyo atashinda mashindano ya wazi ya Ufaransa mnamo mwezi juni basi ataweka rekodi ya kushinda mataji yote makuu msimu huu.
No comments:
Post a Comment