Sir Bobby Charlton, ambae sasa ni Mkurugenzi wa Klabu hiyo, alikuwa Mchezaji mahiri wa Man United na ambae mpaka sasa ndie anashikilia Rekodi ya Ufungaji Bora katika Historia ya Man United akiwa na Mabao 249.
Jina hilo jipya litaanuliwa rasmi hapo Tarehe 2 Aprili 2016 mbele ya Watazamaji 75,000 wakati wa Mechi ya Man United na Everton ambapo pia watakuwepo Watu muhimu katika maisha ya Lejendari huyo.
Sir Bobby Charlton alijiunga na Man United kama Mchezaji Mwanafunzi Mwaka 1953 na kuanza kucheza Mechi yake ya kwanza kabisa Oktoba 1956 ambapo alicheza Jumla ya Mechi 758 hadi anastaafu.


No comments:
Post a Comment