Mchezo huo namba 3, unatarajiwa kuchezwa siku ya Ijumaa saa 10 kamili jioni katika uwanja wa Azam Complex uliopo Chamazi, huku kiingilio cha juu kikiwa shilingi elfu tatu kwa jukwaa kuuu.
Waamuzi wa mchezo huo ni Lidya Tafesse, akisaidiwa na Yehuzewdubizua Yehuw, Tsige Sisay, Woinshetkassaye Abera kutoka nchini Ethiopia, huku Kamisaa wa mchezo huo Geneviev Kanjika akitoka Congo DR wote wanatarajiwa kuwasili siku ya Alhamisi mchana kwa shirika la ndege la Kenya (KQ).
Aidha Kocha Nasra amewaomba wadau wa mpira wa miguu nchini na watanzania wote kwa ujumla, kujitokeza uwanjani siku ya Ijumaa kuja kuwapa sapoti katika mchezo huo, ambapo watakua wakiwakilisha na kupeperusha bendera ya Tanzania.
IMETOLEWA NA TFF
No comments:
Post a Comment