José, Raia wa Ureno mwenye Miaka 53 na ambae ametwaa Makombe 22 tangu 2003, amefundisha Klabu kadhaa kubwaa Ulaya na kutwaa Mtaji katika Nchi 4 tofauti (Portugal, England, Italy na Spain) ikiwa pamoja na kutwaa UEFA CHAMPIONS LIGI, mara 2 akiwa na FC Porto 2004 na Inter Milan 2010.
Akitangaza rasmi uteuzi huu, Makamu Mwenyekiti Mtendaji wa Man United Ed Woodward, alisema: “Jose ni Meneja Bora kabisa kwenye Gemu hivi sasa. Ametwaa Mataji na kuhamasisha Wachezaji katika Nchi kadhaa Ulaya na pia anaijua Ligi Kuu England nje ndani ambako ametwaa Ubingwa mara 3! Namkaribisha Manchester United!”
Zlatan Ibrahimovic kutua nae Old Trafford
AKIONGEA na MUTV, Kituo cha TV cha Manchester United mara baada ya kusaini Mkataba wa Miaka mitatu kuwa Meneja mpya, Jose Mourinho ameserma atafanya kila awezalo kuirejesha Man United kileleni mwa Soka la Dunia.
Aliongeza: “Nadhani hili limekuja wakati muafaka kwa sababu Manchester United ni Klabu kubwa kabisa!”
Mourinho ameeleza: “Nakumbuka tulishinda Old Trafford na Real Madrid [UEFA CHAMPIONS LIGI 2012/13 Raundi ya Mtoano ya Timu 16] na nikasema Timu bora ilifungwa na Real Madrid hawakufurahia hilo!”
No comments:
Post a Comment