Hii itakuwa ni kama marudio ya Fainali ya UCL ya Mwaka ambayo Real walishinda 4-1 katika Dakika za Nyongeza 30 baada ya kusawazisha Bao Bao na kupata Sare ya 1-1 katika Dakika za Majeruhi za Dakika 90 za kawaida.
Hii ni gemu ambayo upande wowote unaweza kushinda lakini ukichukulia kwa uzoefu, Real wako mbele kwa vile wana Mataji 10 ya Ulaya baada ya kutinga Fainali mara 14 wakati Atletico hawajawahi kutwaa Taji hili baada ya kufika Fainali mara 2 tu na kufungwa zote.

Nguvu kubwa ya Atletico ni Difensi yao ngumu lakini itapata shida sana kuwahimili Ronaldo, Bale na Benzema ambao watakuwa wakilishwa na Viungo mahiri Luka Modric na Toni Kroos.
Real wapo chini ya Lejendari wa France Zinedine Zidane, alietwaa UCL Mwaka 2002 akiwa na Real Madrid in 2002, nah ii ndio kazi yake ya kwanza kama Kocha wa Timu kubwa baada ya kumrithi Rafa Benitez aliefukuzwa Mwezi Desemba.
Atletico wako chini ya Muargentina Diego Simeone ambae enzi zake alikuwa Kiungo Mkabaji wa Shokan a ambae ameiongoza Atletico kuanzia 2012 na kuijenga Timu hii kuwa ya Wachezaji wenye nguvu-kazi kubwa Uwanjani.
No comments:
Post a Comment