Bailly amesaini Mkataba wa Miaka Minne ambao una Kipengele cha kuongeza Miaka Miwili baada ya hapo.
Akiongea baada ya kusaini Mkataba, Bailly alisema: “Ni ndoto iliyotimia kujiunga na Manchester United. Kucheza Soka la kiwango cha juu ndicho ninachotaka. Natka niendelee na naamini kufanya kazi na Jose Mourinho kutanisaidia kuendelea kwa njia sahii na Klabu sahihi.”
Nae Mourinho alizungumza: “Eric ni beki wa kati mwenye Umri mdogo na mwenye kipaji asilia. Ameendelea vizuri hadi Leo na ana uwezo kupanda zaidi!”
No comments:
Post a Comment