Jumatano Sweden inaivaa Belgium katika Mechi yao ya mwisho ya Kundi E na Gemu hiyo inaweza kuwa ya mwisho kuichezea Nchi yake.
Ibrahimovic ameeleza: "Nasikia fahari kwa yote niliyofikia na Siku zote nitakuwa na Bendera ya Sweden!"
Manchester United inahusishwa sana kuwa ndio Klabu anayokwenda Straika huyo mwenye Miaka 34 baada ya kuwa Mchezaji huru kufuatia Mkataba wake na Paris St-Germain kumalizika mwishoni mwa Mwezi huu.
Sweden watatupwa nje ya EURO 2016 ikiwa watashindwa kuifunga Belgium kwenye Mechi ya Kundi E lakini wakishinda watasonga Raundi ya Mtoano ya Timu 16.
Msimamo Kundi E:
Mechi za Mwisho za Makundi
Jumatano Juni 22
KUNDI F, Iceland v Austria (1900, Stade de France)
KUNDI F, Hungary v Portugal (1900, Stade de Lyon)
KUNDI E, Italy v Republic of Ireland (2200, Stade Pierre Mauroy)
KUNDI E, Sweden v Belgium (2200, Stade de Nice)
No comments:
Post a Comment