
Hivi karibuni Messi alistaafu kuichezea Timu ya Taifa ya Nchi yake Argentina baada ya kupoteza Fainali ya Copa America Centenario huko Marekani walipobwagwa kwa Mikwaju ya Penati na Chile ukiwa ni mlolongo wa Fainali za Mashindano makubwa Manne ya Mchezaji huyo kushindwa kutwaa Taji kubwa.
Na kabla kovu hilo halijapona, hapo Juzi Mahakama ya huko Spain ilimhukumu Kifungo cha Miezi 21 Jela na kuamriwa kulipa Faini ya Euro Milioni 2 baada ya kupatikana na hatia ya Ukwepaji Kodi.
Taarifa rasmi ya Barcelona ilieleza: “Kampeni inawaasa Mashabiki wote wa Barca kuonyesha Imani yao kwa Mchezaji Bora Duniani kwa kumpa sapoti kwenye Mitandao ya Kijamii”
Nae Rais wa Barcelona Josep Maria Bartomeu ametoa sapoti yake kwa kutoa posti ya Twitter "Leo, wale wanaokushambulia wewe wanaishambulia Barca na historia yake. Tutakulinda mpaka mwisho. Tuko pamoja daima!"
No comments:
Post a Comment