Kwa mujibu wa Taarifa yao waliyoitoa kwenye Tovuti yao, Klabu hiyo imethibitisha kuwa baada ya Mazungumzo mazito Mkhitaryan, mwenye Miaka 27, atahamia Old Trafford.
Staa huyo alikuwa amebakiza Mwaka Mmoja tu kwenye Mkataba wake.
Inaaminika Dau la Uhamisho la Mkhitaryan ni Pauni Milioni 23.6 na anakuwa Mchezaji wa 3 kujiunga na Man United chini ya Meneja Mpya Jose Mourinho katika kipindi hiki.
Wengine waliosainiwa na Man United ni Eric Bailly na Zlatan Ibrahimovic.
Msimu uliopita, Mkhitarayn aliifungia Dortmund Bao 18.
No comments:
Post a Comment