Balotelli, mwenye Miaka 25, alikuwa huko kwao Italy Msimu uliopita akichezea AC Milan lakini hivi sasa amerejea Liverpool akiwa Mazoezini kujitayarisha kwa Msimu mpya.
Meneja huyo Mjerumani amesema: “Hajafikia kiwango cha kuweza kugombea Nafasi moja au mbili na Wachezaji Wanne au Watano. Lazima tupate suluhisho na itatokea Klabu inayomtaka Balotelli mpya.”
Akiwa na AC Milan Msimu uliopita, Balotelli alifunga Bao 3 tu katika Mechi 23 na kuachwa Timu ya Taifa ya Italy iliyocheza Fainali za EURO 2016 ambazo zilikwisha Jumapili iliyopita.
No comments:
Post a Comment