Mbali ya kuwa ni Mechi kati ya Mahasimu wakubwa huko England, Mechi hii pia inawakutanisha wapinzani wawili wakiongoza Timu zao za England na kukutana uso kwa uso kwa mara ya kwanza.

Hii itakuwa Mechi ya Pili kwa kila Timu za majaribioa kwa ajili ya Msimu mpya ambapo wote walifungwa katika Mechi za za kwanza.
City walichapwa 1-0 na Bayern Munich wakati Man United ikifungwa 4-1 na Borussia Dortmund.
Kihistoria Man United wako mbele ya City katika Mechi zao 171 walizocheza kati yao kwa kushinda Mechi 71 dhidi ya 49 za City.
Kwenye Mechi yao ya mwisho waliyokutana huko Etihad Stadium Mwezi Machi, Marcus Rashford ndie aliefunga Bao la ushindi na kuwapa Man United ushindi.
No comments:
Post a Comment