Jaji Thokozile Masipa amepunguza hukumu hiyo kutoka miaka 15 kutokana na muda ambao Pistorius amekuwa kizuizini na pia kutokana na ulemavu wake.
Wakati wa kusikilizwa kwa kesi hiyo, Pistorius aliambia Mahakama kuwa alimpiga risasi Steenkamp kwa makosa akidhani kuwa ni mtu aliekuwa amevamia nyumba yake.
Steenkamp alipigwa risasi mara nne akiwa nyuma ya mlango wa choo usiku wa siku maarufu ya wapendanao ya Valentines mwaka wa 2013.
Waongoza mashitaka wamedai kuwa Pistorius alimuuwa Steenkamp kwa makusudi.
No comments:
Post a Comment