
Brazil walianza Mechi hii kwa kishindo kikubwa pale Kepteni wao Neymar alipofunga Bao lao la kwanza baada ya Sekunde 14 tu tangu Mechi ianze ikiwa ni Historia kwa Olimpiki kwa Bao la haraka kiasi hicho.
Neymar aliweza kurudi tena Uwanjani lakini muda mfupi baadae akakaa chini kwa maumivu na kutolewa tena nje lakini akaweza kurudi tena na kuendelea tena na Mechi.
Hadi Mapumziko Brazil 3 Honduras 0.
Kipindi cha Pili Brazil walipiga Bao 3 nyingine za Dakika za 51, 79 na 90 ambalo lilikuwa la Penati.
Brazil sasa watacheza Fainali na Mshindi kati ya Nigeria na Germany ambao wanacheza baadae Leo.
No comments:
Post a Comment