BOSI wa Nice Lucien Favre ameungama kwamba Mario Balotelli sasa amezidi matarajio yao baada ya Jana kupiga tena Bao 2 kwenye Mechi na Monaco ya Ligi 1 huko France.
Hiyo ni Mechi ya pili mfululizo kwa Balotelli kufunga Bao baadavya Jana Nice kuwachapa Monaco 4-0 katika Dabi ya Riviera na kukaa kileleni mwa Ligi 1 wakiwa juu ya Mabingwa Watetezi Paris Saint-Germain.
Baada ya Gemu hiyo Kocha Favre alisema: "2-0 toka kwa Balotelli zilikuwa ni muhimu na zilitupa morali ya kujiamini. Mario ni muhimu kwetu kwani anatoa kina kwenye Gemu yetu. Sasa anapaswa kuendelea hivi hivi."
Kocha huyo aliendelea: "Baada ya Miaka kadhaa migumu kwake sasa anaweza kurejea kileleni. Tutajaribu kumsaidia ili aimarike zaidi!"
Aliongeza: "Bao 4 Gemu 2? Sikutegemea hilo!"
Hiyo ni Mechi ya pili mfululizo kwa Balotelli kufunga Bao baadavya Jana Nice kuwachapa Monaco 4-0 katika Dabi ya Riviera na kukaa kileleni mwa Ligi 1 wakiwa juu ya Mabingwa Watetezi Paris Saint-Germain.
Baada ya Gemu hiyo Kocha Favre alisema: "2-0 toka kwa Balotelli zilikuwa ni muhimu na zilitupa morali ya kujiamini. Mario ni muhimu kwetu kwani anatoa kina kwenye Gemu yetu. Sasa anapaswa kuendelea hivi hivi."
Kocha huyo aliendelea: "Baada ya Miaka kadhaa migumu kwake sasa anaweza kurejea kileleni. Tutajaribu kumsaidia ili aimarike zaidi!"
Aliongeza: "Bao 4 Gemu 2? Sikutegemea hilo!"
No comments:
Post a Comment