
Msimu huu, chini ya Meneja mpya Pep Guardiola, Toure amecheza Mechi moja tu na ni ile ya Marudiano dhidi ya Steau Bucharest ambayo ilikuwa Mechi ya Raundi ya Mwisho ya Mchujo ya UCL.
City waliibwaga Steau Bucharest kwa kuichapa 5-0 katika Mechi ya kwanza na 1-0 kwenye Mechi ya pili na kutinga Makundi ya UCL ambapo wako Kundi moja pamoja na Borussia Monchengladbach, Celtic na Barcelona.
Tangu atue Guardiola, City imewaondoa kwa Mkopo Joe Hart, Wilfried Bony, Samir Nasri, Eliaquim Mangala na Jason Denayer na ilidhaniwa nae Toure atang’oka hasa baada ya Guardiola kumuuza Mchezaji huyo wa Ivory Coast walipokuwa wote huko Barcelona na kuhamia City Mwaka 2010.
Toure, mwenye Miaka 33, ametwaa Ubingwa wa England mara 2, FA CUP na Kombe la Ligi mara 2 akiwa na City.
Makipa:
Claudio Bravo, Willy Caballero
Mabeki:
Bacary Sagna, Vincent Kompany, Pablo Zabaleta, Aleksandar Kolarov, Gael Clichy, John Stones, Nicolas Otamendi
Viungo:
Fernando, Raheem Sterling, Ilkay Gundogan, Jesus Navas, Kevin De Bruyne, Fabian Delph, Leroy Sane, David Silva, Fernandinho
Mafowadi:
Nolito, Sergio Aguero, Kelechi Iheanacho
No comments:
Post a Comment