Msimu huu mpya Ronaldo, ambae ndie Mchezaji Bora Barani Ulaya, hajacheza hata Mechi moja ya Klabu yake Real Madrid na alirejea Mazoezini baada ya Real kutwaa UEFA SUPER CUP walipoibwaga Sevilla mapema Agosti na pia kuzikosa Mechi mbili za La Liga ambazo zote Real walishinda.
Huenda Zidane akampa muda Ronaldo Uwanjani ili kumjenga polepole baada ya hivi karibuni kuzidisha kasi ya Mazoezi baada ya kupona Goti lake.
Kwenye La Liga, Real, Barca na Las Palmas ndizo Timu pekee zenye Pointi 6 baada ya kushinda Mechi zao zote 2 za kwanza za Msimu mpya na Ligi hiyo kusimama kwa Wiki 2 kupisha Mechi za Kimataifa.
LA LIGA
Ratiba:
Ijumaa Septemba 9
2145 Real Sociedad v RCD Espanyol
Jumamosi Septemba 10
1400 Celta de Vigo v Atletico de Madrid
1700 Real Madrid CF v Osasuna
1915 Malaga CF v Villarreal CF
1915 Sevilla FC v Las Palmas
2130 FC Barcelona v Deportivo Alaves
Jumapili Septemba 11
1300 Sporting Gijon v CD Leganes
1700 Valencia C.F v Real Betis
1915 Granada CF v SD Eibar
2130 Deportivo La Coruna v Athletic de Bilbao
No comments:
Post a Comment