Halsey, ambae alistaafu Urefa Mwaka 2013, aliibua tuhuma hizo kwenye mabishano Mtandaoni Twitter walipozungumzia kushitakiwa kwa Fowadi wa Man City Sergio Aguero ambae alifunguliwa Mashitaka na FA baada ya Refa Andre Marinner kukiri kutoona tukio la Aguero kumpiga Kipepsi Winston Reid kwenye Mechi ya Ligi Kuu England kati ya City na West Ham.
Kwa mujibu wa Kanuni huko England, ikiwa Refa atabainisha hakuona tukio kama hilo basi Mchezaji Mhusika hufunguliwa Mashitaka na
FA, na baada kupitia Mkanda wa Video wa Tukio hilo kama la Aguero na kuamua kulipeleka kwa Jopo Huru la Marefa Watatu wa zamani ambao kwa pamoja wakiridhika kuwa Kosa hilo lilistahili Kadi Nyekundu kama Refa angeliliona na hivyo FA kuwajibika kumfungulia Mashitaka.
No comments:
Post a Comment