Akiongea kwenye Kipindi cha MUTV, Kituo cha TV cha Man United, Rooney alikiri ni kawaida wao kupondwa kutokana na hadhi yao na kusema: “Hiyo ndio Soka, nadhani. Hatukushinda Gemu 3 na ni wazi kila Mtu ataongea hilo. Tulikuwa na Wiki mbaya, Siku 8 mbaya na tulipoteza Gemu 3 na muhimu ni jinsi tutakavyoibuka upya.”
“Inabidi nitie mkazo, nifanye kazi kwa bidii, kama nilivyokuwa nikifanya maisha yangu yote ya Soka nikifanya juhudi na kujaribu kila kitu kwa faida ya Timu.”
Pia Rooney aligusia ushindi wao wa 3-1 dhidi ya Northampton kwenye Mechi ya Raundi ya 3 ya EFL CUP, Kombe la Ligi, na kusema: “Jana Usiku tulishinda na sasa tuna Gemu 3 za Nyumbani kabla ya mapumziko ya Mechi za Kimataifa na ni muhimu tushinde zote ili Msimu wetu urudi kwenye Reli.”
Kuhusu kupangwa kucheza na Mahasimu wao Man City kwenye Raundi ya 4 ya EFL CUP, Rooney ameeleza: “Kwangu mimi ni Droo safi. Baada ya kilichotokea kwenye Ligi, hii ni nafasi safi kulipa kisasi. Ni Mechi safi Old Trafford!”
Pia Rooney amesema ana hakika Man United itakuwemo kwenye mbio za Mataji Msimu huu hasa kwa vile Meneja wao ni Jose Mourinho.
No comments:
Post a Comment