Awali RBFA ilitoa Posti ya Twitter ikisema Mchezaji huyo aliteguka Enka na baadae kutolewa nyingine ikithibitisha kuvunjika Enka ya Kulia baada uchunguzi wa kina.
Hazard, mwenye Miaka 26, sasa ataikosa Mechi ya Kirafiki kati ya Belgium na Czech Republic itayochezwa Leo usiku na pia ile Mechi ya Kundi lao la Nchi za Ulaya kuwania Nafasi za Fainali za Kombe la Dunia za huko Russia Mwaka 2018.
Hazard aliisaidia sana Chelsea kutwaa Ubingwa wa EPL, LIGI KUU ENGLAND, akifunga Bao 16 katika Mechi 36 alizocheza.
Bado Mchezaji huyu ana Mkataba wa Miaka Mitatu na Chelsea lakini hivi karibuni upo uvumi mkubwa kuhusishwa na kuhamia kwa Mabingwa wa Spain na Ulaya Real Madrid.
EPL itaanza rasmi Agosti 12.
No comments:
Post a Comment