BUKOBA SPORTS

Wednesday, June 7, 2017

FORBES - MAN UNITED YAIPIKU REAL KILELENI TIMU YENYE 'THAMANI KUBWA DUNIANI'!

BAADA Wiki iliyopita KPMG kuwataja Manchester United kuwa ndio Klabu yenye 'Thamani Kubwa' Ulaya, Jana Forbes, Magwiji wa Habari za Biashara, wameiweka Klabu hiyo kileleni mwa Listi yao 'Klabu zenye Thamani Kubwa Duniani' ikithaminiwa kwa Pauni Bilioni 2.86.
Hii ni mara ya kwanza kwa Man United kuongoza Listi hiyo katika Miaka Mitano.

Mabingwa hao wa UEFA EUROPA LIGI wamewatambuka Vigogo wa Spain Barcelona na Real Madrid ambao sasa wapo Nafasi za Pili na za 3 kwenye Listi hiyo.
Kwa mujibu wa Forbes, Barca sasa thamani yao ni £2.82bn na Real, ambao ndio walikuwa Namba Wani kwa Miaka Minne iliyopita, thamani yao ni £2.77bn.
Timu zinazofuatia ni Bayern Munich wenye £2.10bn na Manchester City, ambao sasa wameipita Arsenal, wana £1.61bn.
Timu 6 za EPL, LIGI KUU ENGLAND, zipo kwenye 10 Bora zikiungana na Man United ambazo ni Man City, Arsenal, Chelsea, Liverpool na Tottenham.
Kwa Mwaka 2015/16, Man United ilivuna Mapato ya £593m wakizizidi Barca na Real kwa zaidi ya Pauni Milioni 60.

10 BORA - KLABU ZENYE THAMANI KUBWA DUNIANI:
1) Manchester United - US$3.69bn (£2.86bn)
2) Barcelona - $3.64bn (£2.82bn)
3) Real Madrid - $3.58bn (£2.77bn)
4) Bayern Munich - $2.71bn (£2.10bn)
5) Manchester City - $2.08bn (£1.61bn)
6) Arsenal - $1.93bn (£1.50bn)
7) Chelsea - $1.85bn (£1.43bn)
8) Liverpool - $1.49bn (£1.15bn)
9) Juventus - $1.26bn (£980m)
10) Tottenham - $1.06bn (£820m)

No comments:

Post a Comment