BUKOBA SPORTS

Tuesday, June 6, 2017

UHAMISHO: ARSENAL YAMPATA MPYA NI SEAD KOLASINAC

Look out Eden Hazard! Two stats to get Arsenal fans excited about Sead KolasinacArsenal wamethibitisha Sead Kolasinac atajiunga nao Mwezi Julai kama Mchezaji Huru na kwamba atasaini Mkataba wa muda mrefu baada ya kukamilisha taratibu zote za Uhamisho.
Tangu Mwezi uliopita zilikuwepo habari kuwa Beki huyo wa Kushoto mwenye Miaka 23 atajiunga na Arsenal baada kumaliza Mkataba wake na Schalke ya Germany.
Inaaminika Everton, Manchester City na AC Milan zilitoa Ofa kumchukua Kolasinac, lakini mwenyewe ameamua kujiunga na Arsenal hasa baada kuthibitika Meneja Arsene Wenger atabakia Klabuni hapo baada kusaini Mkataba Mpya wa Miaka Miwili.

Hivi sasa Arsenal inao Mfulbeki wa Kushoto Wawili, Nacho Monreal na Kieran Gibbs ambae sasa amefikia Mwaka wa mwisho wa Mkataba wake. 
Kolasinac aliichezea Germany kwenye Timu za Vijana lakini Mwaka 2013 aliamua kuichezea Timu ya Taifa ya Bosnia and Herzegovina ambako ndiko Wazazi wake walizaliwa na tayari ameshacheza Mechi 17.

No comments:

Post a Comment