BUKOBA SPORTS

Monday, January 29, 2018

CRISTIANO RONALDO AFUNGA MAGOLI MAWILI KWA PENATI


Cristiano Ronaldo amefunga mikwaju ya penati miwili katika kipindi cha kwanza na kuisaidia Real Madrid kuifunga Valencia magoli 4-1 na kupunguza presha ya kutimuliwa kocha wao Zinedine Zidane.
Ushindi huo unaifanya Real Madrid kupunguza pengo lake na wenyeji Valencia kuwa tofauti ya pointi mbili tu, ikiwa na mchezo mmoja mkonono, ingawa bado ipo nyuma kwa pointi 16 na vinara wa La Liga Barcelona.
Valencia ilipata goli lake pekee kupitia kwa Santi Mina, huku magoli mengine ya Real Madrid yakifungwa na Marcelo na Toni Kroos kufunga goli la nne kwa shuti kali la masafa dakika moja kabla ya mpira kumalizika.


Mshambuliaji nyota Cristiano Ronaldo akifunga goli kwa mkwaju wa penati

Mjerumani Toni Kroos akiachia shuti kali na kufunga goli katika dakika ya 89

No comments:

Post a Comment