
Mara baada ya kumfunga goli golikipa wa Kagera Juma Kaseja Bocco ameweka rekodi ya kumfunga Golikipa huyo mabao 10 na kuwa ni mshambuliaji pekee wa Tanzania aliyewahi kufanya hivyo.
Jumatatu aliisaidia Simba kuondoka na alama tatu kwa bao la dakika ya 79 kwa pasi safi ya Sbomari Kapombe baada ya Saidi Ndemla kuifungia Simba bao la kwanza dakika ya 72.
Mbali na mchezo huo Singida wakiwa ugenini mkoani Ruvuma wamelazimishwa sare ya bao 1-1 dhidi ya Majimaji Fc bao la Singida likifungwa na Papy Kambale dk 28 kabla ya winga hatari wa majimaji Peter Mapunda kuisawazishia Majimaji dakika ya 85 na kufanya matokeo kuwa 1-1
No comments:
Post a Comment