BUKOBA SPORTS

Saturday, March 24, 2012

BADO MARADONA NI ZAIDI YA MESSI



                                                         Messi na Maradona
 













              
BUENOS ARIES, ARGENTINA
 
STAA wa zamani wa Real Madrid na timu ya taifa ya Argentina, Jorge Voldano, amesema staa wa Barcelona, Lionel Messi ni mchezaji hatari lakini nyota wa zamani wa Argentina, Diego Maradona alikuwa fundi zaidi.

Messi Jumanne ameweka rekodi ya kuwa mfungaji bora wa muda wote Barcelona baada ya kufunga mabao matatu katika ushindi wa mabao 5-3 wa Barcelona dhidi ya Granada na Voldano anaamini kwamba Messi anaweza kuwa mchezaji bora zaidi kuwahi kutokea duniani.

 

Lionel Messi and Diego Maradona - Greece v Argentia: Group B - 2010 FIFA World Cup

Tunamhukumu Messi kwa maisha yake yote ya soka, wakati Messi bado ana miaka 24 tu. Ukweli kwamba mpaka sasa tumefikia hatua ya kuwalinganisha ni heshima kubwa kwa kile ambacho Messi amefanya, alisema Voldano.
 



Kama tunaweza kuwatofautisha, basi tunaweza kusema Maradona alikuwa fundi zaidi na wa kipekee kama utaangalia urembo katika mchezo. Messi kwa upande mwingine ana madhara zaidi na anacheza vizuri kila siku. Ni hatari kila wakati anapopata mpira. Akiendelea kucheza kama hivi, atamzidi kila mtu, akiwemo Pele.

Jumamosi hii Messi ana nafasi ya kuendeleza idadi yake ya mabao 234 aliyofunga mpaka sasa wakati Barcelona itakapokuwa ugenini kucheza na Mallorca wakati huu ikiifukuza Real Madrid iliyo kileleni kwa tofauti

No comments:

Post a Comment