BUKOBA SPORTS

Tuesday, April 10, 2012

MAKAMU WA RAIS DK. GHARIB BILAL AONGOZA KUAGA MWILI WA STEVEN KANUMBA LEADERS, JIJI LA DAR ES SALAAM LAZIZIMA KWA SIMANZI



msafara wa Makamu wa Rais.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. Gharib Bilal akitoa heshima zake za mwisho kwa mwili wa marehemu Steven Kanumba ulioagwa leo kwenye viwanja vya Leaders jijini Dar es salaam huku viongozi mbalimbali wa Serikali, viongozi wa dini, Wanasiasa, Wanamuziki Waigizaji na watu maarufu wamejitokeza kuuaga mwili wa mwigizaji huo aliyekuwa maarufu zaidi nchini Tanzania na nje ya nje ya nchi pia, Marehemu Steven Kanumba anazikwa mchana huu kwenye makaburi ya Kinondoni jijini Dar es salaam.


Mmoja wa waombolezaji akisidiwa na wafanyakazi wa msalaba mwekundu mara baada ya kuzimia katika msiba huo mkubwa.
Kutoka kulia ni Waziri wa Habari, Vijana , Utamaduni na Michezo Dk. Emmanuel Nchimbi, Ridhiwan Kikwete, Mbunge wa Jimbo la Kinondoni Idd Azzan na waombolezaji wengine wakiwa katika msiba huo.
Kundi maalum lililoandaliwa kwa nyimbo za maombolezo likiimba nyimbo za maombolezo katika katika msiba huo.
Jeneza la mwili wa marehemu Kanumba likiwa limewekwa tayari kwa waombolezaji kutoa heshima zao za mwisho
Ndugu  wa karibu wakielekea sehemu waliyotengewa kukaa.
Askari wa kike wakiweka sawa utaratibu wa waombolezaji kupita katika eneo hilo ili kukaa.
Rais wa Shirikisho la wasanii wa Filamu Saimon Mwakifwamba akizungumza katika msiba huo kutoa salamu zao za rambirambi kwa marehemu Steven Kanumba
Mmoja wa waombolezaji akipitishwa juu juu kwenye vichwa vya waombolezaji ili kupata huduma ya kwanza baada ya kuzirai, katikati anayetazama mbele ni Mussa Kisoky Mkurugenzi wa kampuni ya Sofia Production ya jijini Dar es salaam.
Mwigizaji Steven Jacob kushoto akizungumza  jambo na mbunge wa Maswa Mashariki Mh. John Shibuda katikati.
Mr Mtitu kulia akijadili jambo na mmoja wa waombolezaji wa
Utaratibu unapangwa na wanakamati wa kamati ya mazishi
Gari lililobeba mwili wa marehemu Kanumba linaondoka Leaders kwenda Makaburi ya Kinondoni huku likiwa limezungukwa na waombolezaji.
Umati wa waombolezaji ukiondoka kuelekea makaburi ya Kinondoni.
Jeneza lenye Mwili wa Marehemu,Steven Kanumba likiwasili kwenye Viwanja vya Leaders Club,jijini Dar es Salaam asubuhi hii.  Makamu wa Rais,Dkt. Mohamed Gharib Bilal akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa Marehemu Steven Kanumba asubuhi hii kwenye viwanja vya Leaders Club,Jijini Dar es Salaam.akifuatiwa na Mkewe,Pamoja na Mke wa Rais,Mama Salma Kikwete (mwenye nguo nyeupe kulia). Mh. Joseph Mbilinyi a.k.a Sugu akitoa heshima za mwisho.
Kwaya maalum ikiimba nyimbo za maombolezao katika msimba huo kwenye viwanja vya Leaders

Mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi akipiga salute mbele ya jeneza lenye mwili wa marehemu Steven Kanumba kama ishara ya kumkubali kwake na kutoa heshima kwa marehemu Steven Kanumba.      -     www.bukobasports.blogspot.com

mama mzazi wa Kanumba akiwapungia mkono mashabiki wa mwanae waliokuwa viwanja vya leaders wakiuaga mwili wa marehem

watoto wawili walikuwa aki act na marehem Kanumba wakiingia viwanjani
Mwili wa marehemu ukifikishwa viwanjani tayari kwa kumpa heshima ya mwisho




paparaz nao mhh....... 
Mke wa Rais,Mama Salma Kikwete akiwasili viwanjani hapa.

Viongozi mbali mbali wapo kwenye shughuli hii ya kumuaga marehemu Steveen Kanumba.



Mdogo wa Marehemu Kanumba akiwasili viwanjani hapo.




Dada wa Marehemu Kanumba akisaidiwa kubebwa mara baada ya kuishiwa nguvu wakati akiwasili viwanjani hapa.



Viongozi wakuu wa Serikali.



watu wengi wamehudhulia shughuli hii.


Mwili wa Marehemu ukiwasili uwanjani hapa.

ukipelekwa sehemu maalum iliyoangaliwa.

No comments:

Post a Comment