BUKOBA SPORTS

Monday, April 9, 2012

MSIBANI SINZA KWA KANUMBA LEO MCHANA HUU

 
Kanumba Enzi za uhai wake

 

PUMZIKA KWA AMANI STEVEN KANUMBA THE GREAT

 Ni majonzi makubwa sana kwa Watanzania wote sisi tulimpenda lakini Mungu kampenda zaidi, inauma sana kwa kijana mdogo kama Kanumba kufariki wakati alikuwa bado hajazitima ndoto zake .Mungu ailaze roho ya marehemu Swaiba wangu Steven Kanumba ni mengi sana tuliyoyafanya mimi na wewe katika gurudumu ili la sanaa bila kujali yote yaliyotokea ni kawaida ya binadamu kutoelewana kama Baba na Mama wanafunga ndoa kanisani na wanakula viapo vya utii mbele za Mungu lakini wanagombana na kufikia hatua ya kuachana kwanini ishindikane kwetu ni hali ya kwaida katika maisha binadamu kutofautiana mengi yanazungumzwa juu yangu ila kila kitu mimi namuachia Mungu mimi ni mnyonge siwezi kupambana nanyi mnaoniongelea vibaya maumivu nayoyapata juu yenu Mungu hatowaacha siwezi kuzizuia hisia zenu kuzungumza yale mnayojisikia.

 Muda mfupi tu baada ya kufariki Steven Kanumba akiwa kwenye gari lake la kifahari Lexus tangulia ndugu yangu sisi tuko nyuma yako maana kila nafsi itaonja umauti. Wadau nilikuwa kimya kwa kutowaletea matukio  kwa sababu ya shughuli zilkuwa nyingi sana katika msiba nilikuwa kwenye kamati ya mazishi hivyo sikuwa nikipata muda wa kutosha na sio watu wanavyofikiria jamani hata kama kuna matatizo ndio katika maswala ya msiba hapana jamani mimi sijafikia hali hiyo  yakuwa na roho ya kinyama namna hiyo

 Hapa tukiutelemsha mwili wa marehemu katika hospital ya Muhimbili ni mtu wa kwanza kufika katika eneo la tukio

 Tukimfunika rafiki yetu katika safari yakuelekea mochwali

 Safari yetu ya mwisho binadamu wote mara ya kwanza nilipofika  walikataa kumpokea pale hospital mpaka wapate PF 3 ndipo nilipowasha gari na kwenda Salenda polisi na kuwapata askari watatu  ndipo tukapata fursa ya kwenda kumpuzisha marehemu

 Tukimfunika macho maana yalikuwa wazi kama anasinzia

Macho yakiwa yamefumba baada ya kumfumba

 Msiba tukaupeleka nyumbani kwake Kanumba na umati mkubwa ulikuwepo ukiwa una majonzi makubwa kwa kumpoteza mpendwa wao

 Viongozi mbalimbali wa serikali waliudhuria Mrema wa kati akiingia ni mbunge wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania na alishawahi kuwa waziri wa mambo ya ndani


 Waheshimiwa wakiteta jambo

 Kitabu cha kumbukumbu na picha ya marehemu


 Waziri wa ofisi ya Rais na mausiano Mueshimiwa Steven Wasira akindiaka ujumbe wake kwenye kitabu cha kumbukumbu 

 Waziri Mkuu Peter Kayanza Pinda akiwasili kwenye msibani kwakweli tunawashukuru sana serikali yetu kwa kuweza kutufariji katika kindi kigumu tulichokuwa nacho kwa sasa mmetutia moyo kwakweli

 Mueshimiwa Zito wa kushoto mbunge wa Kigoma mjini naye alikuwepo tunakushukuru sana ndugu yetu


 Waziri Mkuu akiongea na mwenyekiti wa kamati ya mazishi bwana Gabriel Mtitu aliyevalia nguo nyeusi

 wakiendelea kuteta jambo

 Rais wa nchi mueshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete naye akiwasili

 Naye akifikia kwenye kitabu cha kumbukumbu

 Mambo yakiendeleaa.....

 Hapa akiongea jambo na baadhi ya wanakamati ya mazishi

 Mwenyekiti wa Bongo Movie Jb akiteta jambo na Mueshimiwa Rais

 Tunakushukura sana Rais wetu kwa kuja kutufariji

 The Greatest nikimsikiliza Rais

 Hapa akiondoka uku akiwasalimia Wananchi wake

 Poleni sana hayo ni maneno yake Mueshimiwa Rais

 Baada ya kuondoka Rais tukawa tunateta jambo ambalo lilimchekesha sana mtoto wa Rais Riz One Kkikwete
 The Greatest nikiwa katika maojian na mwandishi wa habari

 Mzee Chilo akiongea jambo na Steve Nyerere

Salama Jabir na Madam Ritha wakiwa kwenye majonzi 

Dulla wa Planet Bongo na Salama Jabir










wadau
Ruge akiwa na waheshimiwa
Musa K akiwa amefika kufariji wafiwa
Monalisa,Millen & Ruge





....kama siamini vile ......

No comments:

Post a Comment