Tovuti ya www.azamfc.co.tz imeshuhudia mazoezi ya timu hiyo chini ya kocha Stewart Hall yakiwa katika hali nzuriwachezaji wakijituma kuhakikisha wanakuwa vizuri.
Programu ya ijumaa iliyopita wachezaji wote (isipokuwa wachezaji 8 waliokuwa Taifa Stars) walianza kwa mazoezi yakujifua katika gym ya klabu na baadaye mazoezi ya stamina na mwisho wakamalizia kwa kucheza mchezo wakujipima wao kwa wao.
Mchezo huo ulikua wa kuvutia timu ya kwanza ilikuwa chini ya Abdi Kassim na nyingine ilikuwa inaongozwa naJoseph Owino zote zikatoka sare ya 1-1, magolikipa walikuwa vijana kutoka Azam Academy Aishi Salum na JacksonWandwi.
Baada ya mazoezi kocha Stewart alisema mazoezi yanaendelea vizuri na program imekuwa na manufaa kwawachezaji kwa kuwa wamebadilika tofauti na siku waliyoanza mazoezi.
Alisema wachezaji wa Taifa Stars watajiunga na wenzao siku ya Jumatatu kwa ajili ya kufanya mazoezi ya mwishokabla ya kuanza michuano hiyo Julai 14 itakayohusisha timu kutoka nchi 10 za Afrika Mashariki na Kati.
Wachezaji waliohudhuria mazoezini Aishi, Wandwi, Said Morad, Michael Kipre, Abdi Kassim, Himid Mao, IbrahimShikanda, Luckson Kakolaki, Owino, Jabir Aziz, Abdulhalim Humud, Kipre Tchetche, Abdulghan Gulam, GaudenceMwaikimba, Ibrahim Mwaipopo, Samir Haji Nuhu, George Odhiambo, Khamis Mcha, Zahor Pazi na RamadhanChombo ‘Redondo’.
Mchezaji Wazir Salum hakuudhuria mazoezini kutokana na kusumbuliwa na ugonjwa wa malaria, program yamazoezi wiki ijayo, Jumatatu na Alhamis mazoezi ya gym na uwanjani, Jumanne na Ijumaa uwanjani na siku yaJumatano watafanya mazoezi kwenye fukwe za Coco.
No comments:
Post a Comment