Uhispania, baada ya ushindi huo katika uwanja wa Donetsk usiku wa Jumamosi, sasa itakutana na Ureno katika mechi ya nusu fainali.
Jordi Alba, kwa haraka haraka alifanikiwa kumchenga mlinzi aliyemuandama na kuupiga mpira juujuu, na ambao ulimfikia Xabi Alonso, ambaye pasipo kusita alikuwa ameusubiri kwa makini, na kuusindikiza kwa kichwa hadi wavuni, akiandikisha bao la Uhispania baada ya dakika ya 20 za mchezo.
Kwa kawaida Xabi Alonso huwa hakosi kufunga mikwaju ya penalti inapojitokeza, na katika dakika ya 91, aliweza kufunga bao la pili, na akiuelekeza mpira hadi kona ya lango.
Kwa mbinu hafifu Ufaransa ilijitahidi kuitisha Uhispania, lakini juhudi zao za pekee zilizokaribia kuandikisha bao ni wakati Mathieu Debuchy alipousindikiza mpira kwa kichwa kuelekea wavuni baada ya kupigiwa mpira na Franck Ribery.
Bosi wa spain Vicente Del Bosque akisisitiza jambo kuwa waendeleze mashambulizi goli moja halitoshi..
Kocha wa Ufaransa Laurent Blanc akisikilizia moyo na kukumbuka kilichowahi kuwapata hapo nyuma
Adil Rami akichuana na Cesc Fabregas
Hapa Hugo Lloris alidaka mpira uliopigwa na Fabregas
Golikipa wa Ufaransa Lloris akijaribu kuokoa mpira kutoka kwa Fernando Torres
Samir Nasri akimpongeza Jesus Navas mchezaji wa Spain baada ya mtanange kuisha
No comments:
Post a Comment