BUKOBA SPORTS

Saturday, June 16, 2012

EURO 2012: FRANCE WAIFUNGA UKRAINE BAO 2-0 MVUA YASIMAMISHA MTANANGE KWA SAA MOJA!



France jana wamepata ushindi wao wa kwanza kwenye Kundi D la Fainali za EURO 2012 walipowafunga Wenyeji Ukraine bao 2-0 kwenye Mechi iliyochezwa huko Mjnini Donetsk, Ukraine na kusimamishwa baada ya Dakika 4 tu tangu ilipoanza baada ya kuanguka Mvua kubwa ikiambatana Radi.
Mechi hiyo iliendelea tena baada ya Saa moja na kuifanya Mechi nyingine ya Kundi D kati ya England na Sweden icheleweshwe kuanza kwa Robo Saa.
Bao za France zilifungwa na Jeremy Menez, katika Dakika ya 53 na Yohan Cabaye, Dakika ya 56, huku zote zikitengenezwa na Karim Benzema.
France ndio wanaongoza Kundi D wakiwa na Pointi 4 na wanafuata Ukraine wenye Pointi 3, England Pointi 1 na Sweden hawana hata Pointi.
France watacheza Mechi yao ya mwisho ya Kundi D hapo Jumanne Juni 19 dhidi ya Sweden.
Rain stops play: Both sets of players are lead back to the dressing rooms after play was suspended after five minutes
mvua iliwasimamisha kwa muda wa dakika tano baada ya hapo refa akasimamisha mtanange
       

 Samir Nasri (kushoto) wa France na Taras Mikhalik (kulia)wa Ukraine wakichuana
Under cover: Stands were quickly deserted in the stadium while some fans used ponchos and umbrellas in an attempt to keep dry
Mvua kali ilinyesha na kuwafanya mashabiki kurushia
Give me shelter: Ukrainian fans brave the weather as driving rain hots the stadium
mashabiki wa Ukraine watatu wakiendelea kufurahia kwa mvua na hatimaye mwisho wa mechi kufungwa
Storm hit: France and Ukraine made a quick exit from the field after the conditions became unplayable
Baada ya kuona mvua inazidi wachezaji walikatisha mchezo kwa saa moja kwanza
VIKOSI:
Ukraine: Pyatov; Gusev, Khacheridi, Mikhalik, Selin; Yarmolenko, Tymoshchuk, Nazarenko, Konoplyanka; Shevchenko, Voronin.
Akiba: Koval, Kucher, Garmash, Aliev, Shevchuk, Rotan, Milevskiy, Seleznyov, Rakitskiy, Butko, Devic, Goryainov.
France: Lloris; Debuchy, Rami, Mexès, Clichy; Cabaye, Diarra; Menez, Nasri, Ribéry; Benzema,
Akiba: Mandanda, Evra, Valbuena, Giroud, Matuidi, Reveillere, Malouda, M'Vila, Martin, Ben Arfa, Koscielny, Carrasso.
Refa: Björn Kuipers (Netherlands)


RATIBA:
----------------------
Jumamosi, Juni 16
KUNDI A
Saa 3 Dak 45 Usiku
Wroclaw, Poland
Czech Republic v Poland
Warsaw, Poland
Greece v Russia
---------------------
Jumapili, Juni 17
KUNDI B
Saa 3 Dak 45 Usiku
Kharkiv, Ukraine
Portugal v Holland
Lviv, Ukraine
Denmark v Germany
---------------------
Jumatatu, Juni 18
KUNDI C
Saa 3 Dak 45 Usiku
Gdansk, Poland
Croatia v Spain
Poznan, Poland
Italy v Republic of Ireland
-------------------------
Jumanne, Juni 19
KUNDI D
Saa 3 Dak 45 Usiku
Donetsk, Ukraine
England v Ukraine
France v Sweden

No comments:

Post a Comment